• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mipango na Takwimu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Afya
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • maji
    • Elimu
    • Watumishi
    • Kilimo
    • Afya
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti
    • Taratibu
    • Taarifa za Fedha
      • Taarifa ya makisio ya Mapato
      • Taarifa ya Mapato Halisi
      • Taarifa ya Matumizi
      • MTEF
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba

Wawili waswekwa rumande kusuasua miradi ya maji Rombo

Posted on: January 24th, 2020

Watu wawili,Godson Josea -Msimamizi wa mradi wa maji wa Shimbi Mashariki na Mhandisi Amos Thomas walio chini ya Mkandarasi  HECO SANMARK (T) LTD  wanashikiliwa na jeshi la polisi  mpaka Mkandarasi huyo atakapojisalimisha kwenye uongozi wa wilaya.

Maamuzi hayo yamefanywa na Naibu waziri wa Maji Jumaa Aweso baada ya kufika katika mradi wa maji Shimbi Mashariki na kukuta mradi ulioanza toka mwaka 2013 haujakamilika na mkandarasi  ambaye amekwishalipwa fedha na serikali kiasi cha shilingi milioni 100 hayupo eneo la mradi, huku kukiwa na malalamiko ya vibarua kutokulipwa fedha zao.

Aidha Naibu Waziri Aweso amemuagiza Mhandisi wa RUWASA Joseph Mcharo  kuhakikisha anafuata taratibu za kisheria  na kuvunja mkataba na HECO SANMARK (T) LTD  pindi atakapojisalimisha  ili asilimia 12 zilizobaki za mradi kukamilika zifanywe na wataalamu wa Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi Wa Mazingira (RUWASA)Wilaya ya  Rombo  .

Ameongeza kuwa mbali na kushughulikia suala la vibarua kulipwa fedha zao , pia RUWASA wanatakiwa kuhakikisha mzabuni wa  pampu za maji analipwa fedha yake na pampu ziwashwe ili wananchi wa eneo hilo wapate huduma maji.

Mhandisi  Mcharo  amesema kuwa mradi wa maji Shimbi Mashariki wenye thamani ya shilingi milioni 887.4 umeshatekelezwa kwa asilimia 88 huku Mkandarasi akiwa amekwishalipwa kiasi cha zaidi ya milioni 400 na anadai kiasi cha shilingi milioni 86 tu.

Amesema sababu kubwa wanayoitoa wakandarasi ya kuchelewa kukamilisha miradi ni kutolipwa madai yao kwa wakati , na pindi wanapoandikia madai yao wanasimamisha ujenzi mpaka walipwe fedha zao ndio waendelee na kazi.

Vilevile Naibu Waziri Aweso  alitembelea mradi wa maji katika kijiji cha  Leto wenye thamani ya shilingi milioni 927.9 ambao nao pia haujakamilika kitu kinachosababisha wanakijiji wa eneo hilo kwenda kuchota maji nchi jirani ya Kenya.


Matangazo

  • MATOKEO YA USAHILI WA WALIOOMBA KAZI YA KUKUSANYA MAPATO NA KAZI YA USAFI August 27, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO June 14, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA August 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA July 16, 2024
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • Ona Zote

Video

Maafisa Elimu Kata wakizifanyia Majaribio Pikipiki
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Muundo wa Halmashauri
  • Wasiliana Nasi Kwa
  • Miladi iliyokamilika

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • MFUMO WA TAUSI
  • Ffars
  • Tamisemi
  • Idara ya Takwimu (NBS)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Rombo District Council,Mkuu Bomani Street

    Sanduku la Posta: P.o Box 52,Mkuu,Rombo

    Simu: 027-2757101

    Simu ya Mkononi: 027-2757101

    Barua Pepe: ded@rombodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright@2019Rombodc.all rights reserved