• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mipango na Takwimu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Afya
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • maji
    • Elimu
    • Watumishi
    • Kilimo
    • Afya
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti
    • Taratibu
    • Taarifa za Fedha
      • Taarifa ya makisio ya Mapato
      • Taarifa ya Mapato Halisi
      • Taarifa ya Matumizi
      • MTEF
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba

Wanafunzi Mjionee Huruma DC Rombo

Posted on: August 2nd, 2018

Mkuu wa wilaya ya Rombo Agness Hokororo awaasa wanafunzi wa kike wajionee huruma wasiharakie mambo yasiyowahusu kabla ya wakati, japokuwa kuna kesi chache za ubakaji lakini wengi wamekuwa wakienda maeneo yasiyowahusu na matokeo yake wanavuna kile walichokipanda.

Hayo aliyasema alipokuwa akihutubia katika maadhimisho ya juma la Elimu wilaya ya Rombo katika Viwanja vya shule ya sekondari Mkuu.

Aidha aliwaagiza walimu kuwajengea watoto wa jinsia zote uwezo kuanzia darasa la awali na kuendelea ili waweze kujua haki zao, maeneo wasiopaswa kushikwa, na vitendo wasivyopaswa kufanyiwa ili yakiwatokea waripoti kwa walimu wao.

Waratibu elimu kata na wakuu wa shule kuhakikisha mtoto anayethibitishwa na daktari kuwa na ujauzito asiondoke eneo la shule kabla ya kuripotiwa kituo cha polisi na awe amemtaja mhusika kabla hajarudi nyumbani ili kutovujisha siri na mtuhumiwa kutoroka.

“Wazazi,walezi, ,wadau wa elimu, wanafunzi wenyewe pamoja  na serikali hatuzungumzi lugha moja katika kukemea na kupinga vitendo vya ukatili kwa watoto kitendo kinachosababisha kukatiza masomo kwa watoto wa kike na kushuka kwa kiwango cha taaluma”alisema Hokororo.

DC Hokororo ameliagiza jeshi la polisi kutosita kuwaweka ndani wazazi wa pande zote mbili iwapo wakishirikiana kuficha mhusika wa ujauzito mpaka pale atakapopatikana na kufikishwa mahakamani.

Afisa Elimu Sekondari(W) Petronila Wakurila amesema kuwa tatizo ya ulawiti ni kubwa kwa shule za msingi  na tatizo la mimba za utotoni ni kubwa zaidi kwa shule za sekondari vitu vinavyoathiri saikolojia yao na kuhatarisha maendeleo ya taaluma pamoja na makuzi.

Aliongeza kuwa kwa kushirikiana na Idara ya Maendeleo ya jamii pamoja na Idara ya Afya wanaendelea kutoa elimu kwa jamii itakayosaidia kutokomeza matatizo ya ulawiti na mimba za utotoni.

Wilaya ya Rombo inakabiliwa na tatizo la wanafunzi kukatisha masomo kutokana na kupata ujauzito wakiwa shuleni ambapo kwa mwaka 2016 mimba 72 ziliripotiwa,mwaka 2017 mimba 64 ziliripotiwa na mwaka 2018 mimba 31 zimesharipotiwa japo jitihada kubwa ya kuondoa/ kupunguza mimba za utotoni zinafanywa bado hayajapatikana matunda ya kutosha.



Matangazo

  • MATOKEO YA USAHILI WA WALIOOMBA KAZI YA KUKUSANYA MAPATO NA KAZI YA USAFI August 27, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO June 14, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA August 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA July 16, 2024
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI.

    May 29, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • Ona Zote

Video

Maafisa Elimu Kata wakizifanyia Majaribio Pikipiki
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Muundo wa Halmashauri
  • Wasiliana Nasi Kwa
  • Miladi iliyokamilika

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • MFUMO WA TAUSI
  • Ffars
  • Tamisemi
  • Idara ya Takwimu (NBS)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Rombo District Council,Mkuu Bomani Street

    Sanduku la Posta: P.o Box 52,Mkuu,Rombo

    Simu: 027-2757101

    Simu ya Mkononi: 027-2757101

    Barua Pepe: ded@rombodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright@2019Rombodc.all rights reserved