• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mipango na Takwimu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Afya
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • maji
    • Elimu
    • Watumishi
    • Kilimo
    • Afya
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti
    • Taratibu
    • Taarifa za Fedha
      • Taarifa ya makisio ya Mapato
      • Taarifa ya Mapato Halisi
      • Taarifa ya Matumizi
      • MTEF
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba

Shida ya Maji Rombo yaiweka Kiliwater Kitanzini

Posted on: February 6th, 2019

Baraza la madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Rombo limeazimia kuvunja mkataba baina ya Halmashauri na Kampuni ya maji ya Kiliwater inayosimamia na kuendesha miradi ya maji Rombo kwa kushindwa kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Rombo.

Sambamba na hilo baraza limetoa maagizo kwa Mkurugenzi Mtendaji  kuunda kamati maalumu itakayokwenda kuonana na Waziri wa maji ili kuunda mamlaka ya maji Rombo itakayokua inapata ruzuku serikalini ili kuimarisha huduma ya maji kwa wananchi.

Maamuzi hayo yamefikiwa baada ya baadhi ya madiwani kuwasilisha hoja maalum katika baraza  la madiwani lililofanyika mnamo tarehe 05.02.2019 katika ukumbi wa Halmashauri na Baraza la Madiwani kujadili hoja hiyo kwa kina.

Aidha Mhandisi wa Maji (W) John Msengi amelieleza baraza la madiwani kuwa Kampuni ya Kiliwater ipo kwa ridhaa ya warombo wenyewe baada ya serikali kujiondoa katika majukumu ya uendeshaji wa miradi ya maji moja kwa moja na kuwataka wananchi wenyewe waamue na wakaamua kuipa dhamana hiyo kampuni ya Kiliwater.

Akifafanua hilo amelieleza baraza la madiwani kuwa kabla ya mabadiliko ya sera mwaka 1995 serikali ilikuwa na majukumu makuu matatu ambayo ni sera na mipango, pili ni ujenzi wa miradi ya maji, upanuzi na ukarabati mkubwa na tatu ni uendeshaji na usimamizi  ambapo baada ya mabadiliko ya sera  Wizara iliona serikali inapata gharama kubwa kuendesha moja kwa moja na kuanzisha sera ya kuundwa vyombo huru vitakavyosaidia kusimamia na kuendesha miradi ya maji kama vile mamlaka , watu binafsi na makampuni .

Baada ya mchakato wa kuunda vyombo hivyo  kukamilika serikali ilihamisha jukumu la tatu la uendeshaji na usimamizi kwa kampuni pamoja na kuwapa  vitendea kazi, na serikali kuendelea kuisimamia Kampuni kwa utaratibu na makubaliano waliyoyaweka katika andiko .

Hata hivyo Mhe Gaston Mtuta Diwani wa Kata ya Reha ambae ndiye aliyewasilisha hoja hiyo alisema kuwa kampuni ya Kiliwater haijawahi kukaguliwa na mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG), haina wafanyakazi wenye ujuzi wa kutosha na haiwajibiki kwa wananchi.

Ameongeza kuwa kampuni inazalisha maji lita za ujazo 18,000 kwa siku kipindi cha kiangazi na lita 22,000 kipindi cha masika wakati hali halisi ya mahitaji ya huduma hiyo kwa wananchi ni lita za ujazo 40,000 kwa siku hii inaonesha wazi kampuni haiwezi kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Rombo.

Naye Meneja wa Kiliwater (W) Prosper Kessy ameikanusha madai ya kampuni kutowajibika kwa wananchi ambapo amesema kuwa vikao vinafanyika kila mwaka na kamati za maji katika kila kijiji katika tarafa husomewa taarifa mbalimbali za utekelezaji, mipango ya kampuni pamoja na changamoto ,vyote vinawekwa wazi na wananchi wanashiriki kikamilifu.

Aidha amelihakikishia Baraza la Madiwani kuwa  Kampuni ya Kiliwater ina wataalamu wa kutosha wenye elimu kubwa na wanafanya kazi kwa weledi mkubwa. Na taarifa zote za utekelezaji wa majukumu huwasilishwa kuanzia ngazi ya  Halmashauri,mkoa  mpaka Wizara.

Kessy amesisitiza kuwa kampuni ipo kutoa huduma na sio kibiashara na kama utaratibu wa Makampuni ulivyo ni budi kukaguliwa na wakaguzi huru wa hesabu za Fedha na kutolewa taarifa , na hilo limekuwa likifanyika kwa Kampuni ya Kiliwater toka ilipoanzishwa.

Pamoja na hayo Kessy amesema ili kampuni ifanye vizuri inatakiwa kupata ushirikiano mzuri kutoka kwa wadau wote wa maji ikiwa ni pamoja na kuwa walinzi wa miundombinu ya maji na wao kama Kampuni watajitahidi kuboresha huduma ya maji kwa kutumia rasilimali walizonazo.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAHILI WA WALIOOMBA KAZI YA KUKUSANYA MAPATO NA KAZI YA USAFI August 27, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO June 14, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA August 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA July 16, 2024
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • Ona Zote

Video

Maafisa Elimu Kata wakizifanyia Majaribio Pikipiki
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Muundo wa Halmashauri
  • Wasiliana Nasi Kwa
  • Miladi iliyokamilika

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • MFUMO WA TAUSI
  • Ffars
  • Tamisemi
  • Idara ya Takwimu (NBS)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Rombo District Council,Mkuu Bomani Street

    Sanduku la Posta: P.o Box 52,Mkuu,Rombo

    Simu: 027-2757101

    Simu ya Mkononi: 027-2757101

    Barua Pepe: ded@rombodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright@2019Rombodc.all rights reserved