• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mipango na Takwimu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Afya
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • maji
    • Elimu
    • Watumishi
    • Kilimo
    • Afya
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti
    • Taratibu
    • Taarifa za Fedha
      • Taarifa ya makisio ya Mapato
      • Taarifa ya Mapato Halisi
      • Taarifa ya Matumizi
      • MTEF
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba

Rombo yajipanga kupunguza utapiamlo

Posted on: November 23rd, 2020

Katika harakati za kupambana na athari za utapiamlo na kuboresha hali ya lishe katika wilaya ya Rombo, kamati ya lishe wilaya  chini ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, imejipanga kutoa elimu ya kutosha kwa wananchi wote kuhakikisha athari za utapiamlo zinapungua.

Akizungumza mara baada ya kufungua kikao cha kamati ya lishe wilaya, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri  ya Wilaya ya Rombo Ndugu Chrispin Mng’anya amesema kuwa ni vyema elimu ya lishe itolewe kwa wamama wanaonyonyesha na  wajawazito ili watoto wanapozaliwa wawe tayari mama zao wanaelewa umuhimu wa lishe bora kwa watoto.

“Siku elfu moja(1000) za mwanzo za maisha ya mtoto ni msingi wa lishe bora kwa mtoto na lishe isipozingatiwa katika muda huo inaathiri ukuaji wa mtoto kimwili na kiakili”, alisema Mng’anya.

Aliongeza kuwa agenda ya lishe iwe ya kudumu kwenye vikao vinavyofanyika katika maeneo yetu ikiwa ni pamoja na uwepo wa timu maalum katika kila ngazi itakayosaidiana na Afisa Lishe kutoa elimu ya lishe kwa jamii.

Naye Mganga Mkuu wa Wilaya, Bw. Boaz Mwaikugile amesema kuwa kutokuwa na mpangilio mzuri wa chakula na lishe kwa ujumla kunaweza kusababisha maradhi mengi katika mwili wa binadamu likiwepo tatizo la utapiamlo.

“Magonjwa mengi yanayowapata binadamu yana uhusiano mkubwa sana na suala la lishe, mbali na tatizo la utapiamlo kuna maradhi kama vile kisukari, shinikizo la damu na mengine mengi”alisema Mwaikugile

Naye Mhandisi wa maji(W) Bw John Msengi ambaye ni mjumbe wa kamati hiyo ameshauri kabla ya kamati kuanza kazi rasmi ya kupambana na utapiamlo ni vema kufanya uchunguzi na kutambua ukubwa wa tatizo la utapiamlo kiwilaya na takwimu zioneshe maeneo yenye shida zaidi ili nguvu kubwa ielekezwe katika maeneo hayo.

Hali ya utapiamlo inasababishwa na ukosefu wa lishe/chakula bora pamoja na maambukizi ya mara kwa mara yanayosababisha mtu kukosa hamu ya kula na kushindwa kula mlo kamili. Wakina mama wajawazito na wanaonyonyesha wapo kwenye hatari zaidi ya ya kupata utapiamlo na watoto wadogo wanaweza kuathirika toka tumboni iwapo mama hakupata lishe bora kabla na wakati wa ujauzito.




Matangazo

  • MATOKEO YA USAHILI WA WALIOOMBA KAZI YA KUKUSANYA MAPATO NA KAZI YA USAFI August 27, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO June 14, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA August 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA July 16, 2024
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • Ona Zote

Video

Maafisa Elimu Kata wakizifanyia Majaribio Pikipiki
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Muundo wa Halmashauri
  • Wasiliana Nasi Kwa
  • Miladi iliyokamilika

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • MFUMO WA TAUSI
  • Ffars
  • Tamisemi
  • Idara ya Takwimu (NBS)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Rombo District Council,Mkuu Bomani Street

    Sanduku la Posta: P.o Box 52,Mkuu,Rombo

    Simu: 027-2757101

    Simu ya Mkononi: 027-2757101

    Barua Pepe: ded@rombodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright@2019Rombodc.all rights reserved