• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mipango na Takwimu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Afya
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • maji
    • Elimu
    • Watumishi
    • Kilimo
    • Afya
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti
    • Taratibu
    • Taarifa za Fedha
      • Taarifa ya makisio ya Mapato
      • Taarifa ya Mapato Halisi
      • Taarifa ya Matumizi
      • MTEF
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba

Pombe zisizo na TBS Rombo, Basi

Posted on: October 5th, 2018

Mkuu wa wilaya ya Rombo Mhe Agnes Hokororo ametangaza mapambano endelevu dhidi ya uzalishaji wa  pombe haramu ya gongo pamoja na pombe za ndizi zisizo na viwango alipokuwa akiongoza kikao cha kamati ya ushauri ya wilaya( DCC) kilichofanyika tarehe 5 octoba mwaka huu .

Akizungumza katika kikao hicho Mhe.Hokororo amevitaka vyombo vya dola kufanya wajibu wao ikiwa ni pamoja na kukagua ikibidi kuzuia uingizwaji wa malighafi zinazotengeneza pombe hizo kwa mfano molasses ambazo huwa zinaingizwa Rombo kwa kisingizio kuwa ni chakula cha ng’ombe ilihali matumizi halisi ni kutengenezea gongo.

"Sisi sote kama  wananchi wenye nia njema na wilaya ya Rombo, basi tushirikiane kwa pamoja kutoa taarifa, kuwakamata ,kuwachukulia hatua na kuwafikisha mahakamani wazalishaji na watengenezaji wa pombe haramu zisizo na TBS", alisema Hokororo

Naye mjumbe mualikwa Bi Faith Sway kutoka WOCHIVI (Women and Child Vision) Taasisi isiyo ya kiserikali inayosaidia kupambana na ulevi uliokithiri, ameshukuru ushirikiano mkubwa anaoupata kutoka kwa mkuu wa wilaya pamoja na Afisa Tarafa ya Tarakea ambapo vijiji vya Mbomai na Kikelelwa vinafanyiwa kazi na taasisi hiyo.

Akitoa mchango wa mawazo katika kikao hicho Bi Faith amesema kuwa ulevi uliokithiri unasababisha matatizo mengi katika jamii ikiwemo ubakaji pamoja na ongezeko la maambukizi ya VVU.

Sambamba na hilo Afisa Tarafa Tarakea Ndg Saburi Uledi aliwasilisha taarifa ya msako uliofanyika mwezi Agosti na Septemba, 2018  na kufanikiwa kukamata mitambo 11 ya kutengenezea gongo pamoja na lita 80 za gongo na kesi tatu tayari zipo mahakamani

Wilaya ya Rombo imeendelea kudhibiti uanzishwaji wa kampuni na viwanda bubu vinavyozalisha  pombe huku ikifanikiwa kuvifungia  viwanda na kampuni katika vijiji vya Shimbi,Lessoroma,Marangu Katangara na Kirongo Chini.



Matangazo

  • MATOKEO YA USAHILI WA WALIOOMBA KAZI YA KUKUSANYA MAPATO NA KAZI YA USAFI August 27, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO June 14, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA August 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA July 16, 2024
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • Ona Zote

Video

Maafisa Elimu Kata wakizifanyia Majaribio Pikipiki
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Muundo wa Halmashauri
  • Wasiliana Nasi Kwa
  • Miladi iliyokamilika

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • MFUMO WA TAUSI
  • Ffars
  • Tamisemi
  • Idara ya Takwimu (NBS)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Rombo District Council,Mkuu Bomani Street

    Sanduku la Posta: P.o Box 52,Mkuu,Rombo

    Simu: 027-2757101

    Simu ya Mkononi: 027-2757101

    Barua Pepe: ded@rombodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright@2019Rombodc.all rights reserved