• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mipango na Takwimu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Afya
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • maji
    • Elimu
    • Watumishi
    • Kilimo
    • Afya
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti
    • Taratibu
    • Taarifa za Fedha
      • Taarifa ya makisio ya Mapato
      • Taarifa ya Mapato Halisi
      • Taarifa ya Matumizi
      • MTEF
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba

Hali ya Mpaka si salama -Waziri Mkuu

Posted on: February 25th, 2019

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amesema kuwa hali ya mpaka baina ya Kenya na Tanzania si salama kwa sababu wananchi wengi wanapenda kutumia njia za panya kuingia na kutoka upande mmoja wa nchi kwenda mwingine.

Katika ziara yake wilayani Rombo mnamo tarehe 23.2.2019 Mhe.  Majaliwa amewaasa wananchi  wa nchi  zote mbili kuwa walinzi wa mpaka huo kwa kuhakikisha wanafuata taratibu pindi wanapotaka kuingia upande wa pili na kuacha kutumia njia za vichochoro ambavyo vinafanya mambo ya hovyo na kuhatarisha usalama wa nchi hizi mbili.

“Hali ya ulinzi na usalama katika mpaka huu wa Holili si nzuri na polisi pekee au Jeshi  pekee haliwezi kuulinda mpaka huu kwa urefu wote, hivyo ni muhimu sana wananchi kwa ujumla wake wa pande zote mbili kuwa walinzi wa mpaka huu kwa kuhakikisha mnapita katika vituo rasmi vilivyowekwa ili kutoa taarifa za kutoka na kuingia”, Mhe.Majaliwa ameyasema hayo akihutubia wananchi katika eneo la Kastamu Holili.

Ameongeza kuwa, Serikali imeona viashiria mbalimbali vinavyoonesha maeneo ya mpakani hayapo salama, kutokana na matukio ya kutisha yanayotokea katika maeneo ya mipakani  nchini, kwa mfano mauaji ya watoto katika mkoa wa Njombe na utekaji wa watoto  na kudai fedha katika wilaya ya Kibondo inayopakana na nchi ya Burundi.

Aidha, Mhe. Majaliwa amesema kuwa  Serikali imejipanga kuimarisha ulinzi na usalama katika maeneo yote ya mipaka , na wanaotumia njia za vichochoroni (njia za panya) kupitisha bidhaa ndio wanaoweka na vitu visivyo halali kama mabomu na bunduki, hivyo yeyote atakayekamatwa anapita njia hizo na mafurushi hata kama ni bidhaa za biashara bila kufuata utaratibu atakamatwa na atashughulikiwa.

Hata hivyo ametumia nafasi hiyo kuwaasa watumishi wa umma hasa maafisa uhamiaji kutojihusisha na vitendo vya  rushwa ambavyo vinasababisha kuruhusu mambo mengi bila kufuata utaratibu kwa sababu nchi zote mbili zipo makini sana katika suala hilo hivyo watumishi wa umma wajiimarishe na  iwapo ikibainika serikali haitaunda tume itashughulika na muhusika papo hapo.

Matangazo

  • MATOKEO YA USAHILI WA WALIOOMBA KAZI YA KUKUSANYA MAPATO NA KAZI YA USAFI August 27, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO June 14, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA August 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA July 16, 2024
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • Ona Zote

Video

Maafisa Elimu Kata wakizifanyia Majaribio Pikipiki
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Muundo wa Halmashauri
  • Wasiliana Nasi Kwa
  • Miladi iliyokamilika

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • MFUMO WA TAUSI
  • Ffars
  • Tamisemi
  • Idara ya Takwimu (NBS)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Rombo District Council,Mkuu Bomani Street

    Sanduku la Posta: P.o Box 52,Mkuu,Rombo

    Simu: 027-2757101

    Simu ya Mkononi: 027-2757101

    Barua Pepe: ded@rombodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright@2019Rombodc.all rights reserved