• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mipango na Takwimu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Afya
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • maji
    • Elimu
    • Watumishi
    • Kilimo
    • Afya
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti
    • Taratibu
    • Taarifa za Fedha
      • Taarifa ya makisio ya Mapato
      • Taarifa ya Mapato Halisi
      • Taarifa ya Matumizi
      • MTEF
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba

WADAU WA ELIMU WAKUTANA KUFANYA TATHMINI YA MATOKEO SEKONDARI 2022-2023

Posted on: March 22nd, 2023

Idara ya elimu, wadau wa elimu pamoja na viongozi mbalimbali wa halmashauri ya wilaya ya Rombo, wamefanikiwa kufanya kikao cha tathmini ya mwenendo wa matokeo ya kidato cha pili na kidato nne. Kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa shule ya saint joseph iliyopo mkuu, Rombo kililenga kufikia ufaulu wa asilimia 100 kwa wanafunzi wa elimu ya sekondari kwakuwa ndipo maarifa ya msingi katika uhai na ufanisi wa maisha ya mwanadamu yalipo.

Moja ya agenda katika kikao hiko kilichohudhuriwa na wadau wa elimu mbalimbali ikiwemo waalimu, waalimu wakuu, wakuu wabodi ya shule, maafisa elimu kata na waheshimiwa madiwani, ilikuwa ni kupata taarifa ya elimu na umuhimu wa wadau wa elimu katika kuhakikisha wanafunzi wanapata kile wanachostahili kupata shuleni.

Hata hivyo kikao hiko kilifanikiwa kuweka makubaliano ya kimkakati ya kuongeza ufaulu kwa mwaka 2023 endapo yatafanyiwa utekelezaji unaoendana na kauli mbiu isemayo “MBINU SHIRIKISHI UWAJIBIKAJI UTAWEZESHA YALIYOSHINDIKANA YAWEZEKANE”.Yafuatayo ni makubaliaono ya kimakakati yaliyopitishwa na wadau wa elimu  ambayo ni pamoja na

  • kuuongeza muda wa wanafuzi kujisomea
  • kuhimiza matumizi ya lugha ya kiingereza katika kuongea na kuandika shuleni
  • kutumia njia shirikishi zenye kujenga umahiri katika ufundishaji na ujifunzaji
  • kuhakikisha mada azote zinafundishwa vizuri, kwa ukamilifu na kwa wakati
  • kufanya tathimini kubaini maeneo yenye changamoto katikaufundishaji
  • kutumia vijitabu vya cira kufanya mapitio ili kubaini dosari zilizojitokeza katika majibu ya watahiniwa
  • kuhimiza ushindani na hamasa baina ya waalimu na wanafunzi katika kujifunza na kufundisha 
  • kuhimiza uandishi sahihi wa insha kwa kuzingatia vigezo vilivyobainishwa
  • kuhimiza michezo na clubs mbalimbali shuleni

Aidha, afisa taaluma sekondari wailaya ambaye  ndiye aliyekuwa  mwenyekiti wa kikao hicho , aliendesha majadiliano na maazimio na wadau hao wa elimu na kusema kuwa, wilaya imejipanga kutoa motisha chanya ya Tsh 5,000/= kwa kila “A” halali, na hadi sasa Tsh 5,000,0000/= zimeshaanza kukusaanywa kwaajili ya zawadi kwa wadau wote wa elimu watakao faulisha kwa ufaulu wa asilimia 100. Lengo la utoaji wa zawadi likiwa ni kuongeza na kuchochea ufaulu kwani tathimini ya mwenendo na hali ya matokeo kiujumla hairidhishi hivyoo amewaasa wadau wote wa elimu kuchukua kwa uzito utekelezaji wa majukumu yao kama wadau wa elimu.

Katika kikao hicho mlw. Charles Daudi Mganga (Kaimu Mkurugenzi) alifanikiwa kutoa nasaa zake  na kuwaasa sana waalimu kujitoa kikamilifu katka kutekeleza majukumu yao kwani  waalimu  ndio wenye mchango mkubwa kuahakikisha ufaulu wa asilimia 100 kama yalivyo malenge.

Hata hivyo naye aliyekuwa mgeni rasmi ambae ni Katibu wa mbunge aliongeza kwa kuwatia moyo wadau wa elimu na kuahidi kuchukuwa changamoto zilizotajwa na wadau wa elimu na  kuwahakikishia atazipeleka mahala husika zipatiwe mwarobaini.

 Hali kadhalika Katika kikao hicho, ,halmashauri ya wilaya ya Rombo kupitia idira ya elimu,  ilifanikiwa kutoa vyeti na zawadi mbalimbali, ikiwemo mitungi ya gesi, sukari na mchele kwa shule zilizofanyanya vizuri, pia kwa shule zilizoonyesha jitihada na mjongeo chanya katika matokeo ya kidato cha pili na  cha nne ya mwaka 2022.

Kwa taarifa zaidi kuhusu tathimini hiyo unaweza ukaipata hapa

Matangazo

  • MATOKEO YA USAHILI WA WALIOOMBA KAZI YA KUKUSANYA MAPATO NA KAZI YA USAFI August 27, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO June 14, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA August 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA July 16, 2024
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • Ona Zote

Video

Maafisa Elimu Kata wakizifanyia Majaribio Pikipiki
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Muundo wa Halmashauri
  • Wasiliana Nasi Kwa
  • Miladi iliyokamilika

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • MFUMO WA TAUSI
  • Ffars
  • Tamisemi
  • Idara ya Takwimu (NBS)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Rombo District Council,Mkuu Bomani Street

    Sanduku la Posta: P.o Box 52,Mkuu,Rombo

    Simu: 027-2757101

    Simu ya Mkononi: 027-2757101

    Barua Pepe: ded@rombodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright@2019Rombodc.all rights reserved