• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mipango na Takwimu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Afya
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • maji
    • Elimu
    • Watumishi
    • Kilimo
    • Afya
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti
    • Taratibu
    • Taarifa za Fedha
      • Taarifa ya makisio ya Mapato
      • Taarifa ya Mapato Halisi
      • Taarifa ya Matumizi
      • MTEF
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba

Wanaume na Hofu ya Kupima VVU

Posted on: September 26th, 2018

Uzinduzi wa kampeni  ya Pima, Jitambue, Ishi  Wilaya ya Rombo ulifanyika  siku ya tarehe 25.09.2018 katika viwanja vya stendi ya mabasi Mkuu ikiwa ni kampeni ya Kitaifa yenye lengo la kufikia asilimia 90 ya watanzania ambao wamepimwa  VVU na kujua hali zao ifikapo mwaka 2020 na kundi la kwanza linalolengwa ni wanaume, likifuatiwa na vijana wa kike kuanzia miaka 15 hadi 25 na kundi la tatu ni wanawake wajawazito.

Katika uzinduzi huo Mkuu wa Wilaya ya Rombo, Mhe.  Agnes Hokororo amewaomba wanaume wa Rombo kujitokeza kwa wingi na kupima  hali zao na kuacha kuwategea wake zao kwasababu ni muhimu katika familia au kaya zetu kuhakikisha kila mmoja wetu ametambua afya yake .

“Takwimu za kitaifa zinaonesha wanaume wamekuwa na muitikio mdogo wa kupima VVU na kuwaachia wanawake hasa  wakinamama  wajawazito jukumu la kupima afya zao na wanapokutwa hawana maambukizi  na wao wanajihakikishia kuwa wako salama kupitia vipimo vya wake zao.” Alisema Hokororo

Aliongeza kuwa kuna faida kubwa ya kujua hali ya afya zetu na iwapo ukikutwa na maambukizi kuanza dawa mapema ni mwili kuweza kupambana na virusi vinavyosababisha UKIMWI  na kufubaa mapema hatimaye kupunguza kiwango cha virusi mwilini.

“Ninachukua fursa hii kuishukuru serikali chini ya Wizara ya Afya, Jinsia , Wazee na Watoto  kwa kubuni na kufanya kampeni hii lakini pia nichukue fursa hii kuwaomba sana viongozi wa dini mbalimbali kusaidia kushawishi waumini wao kupima afya ili kufahamu hali zao”, alimalizia Hokororo

Naye Mratibu wa UKIMWI  Wilaya ya Rombo Dkt Agripina Masao alisema kuwa zoezi la upimaji la kitaifa lenye kauli mbiu ya “Furaha yangu; Pima, Jitambue, Ishi” litaendelea mpaka novemba 30 mwaka huu ambapo kiwilaya tumepewa malengo ya kuhakikisha  tumepima watu 6,689.

Ameongeza kuwa zoezi hili lilianza toka tarehe 17 Septemba  na mpaka tarehe 23 Septemba watu 236 walijitokeza kupima na hakuna na aliyekutwa na maambukizi  na zoezi litaendelea kufanyika mpaka Novemba  30 , 2018 kwenye Vituo vya Afya, Zahanati na Hospitali zote zinazotoa huduma ya kupima VVU.

Lengo kuu la kampeni hii ya kitaifa ni kutekeleza mikakati ya kufikia 90 tatu yaani 909090 ifikapo mwaka 2020, 90 ya kwanza ikiwakilisha asilimia ya watu watakaojitokeza kupima VVU na kujua hali zao za maambukizi, 90 ya pili ni asilimia ya watu waliokutwa na maambukizi na kuanza dawa mara moja, 90 ya tatu ni asilimia ya watu wanaotumia dawa kwa uaminifu ili waweze kuwa na kiwango kidogo cha Virusi Vya UKIMWI.





Matangazo

  • MATOKEO YA USAHILI WA WALIOOMBA KAZI YA KUKUSANYA MAPATO NA KAZI YA USAFI August 27, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO June 14, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA August 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA July 16, 2024
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • Ona Zote

Video

Maafisa Elimu Kata wakizifanyia Majaribio Pikipiki
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Muundo wa Halmashauri
  • Wasiliana Nasi Kwa
  • Miladi iliyokamilika

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • MFUMO WA TAUSI
  • Ffars
  • Tamisemi
  • Idara ya Takwimu (NBS)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Rombo District Council,Mkuu Bomani Street

    Sanduku la Posta: P.o Box 52,Mkuu,Rombo

    Simu: 027-2757101

    Simu ya Mkononi: 027-2757101

    Barua Pepe: ded@rombodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright@2019Rombodc.all rights reserved