• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mipango na Takwimu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Afya
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • maji
    • Elimu
    • Watumishi
    • Kilimo
    • Afya
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti
    • Taratibu
    • Taarifa za Fedha
      • Taarifa ya makisio ya Mapato
      • Taarifa ya Mapato Halisi
      • Taarifa ya Matumizi
      • MTEF
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba

Historia

Eneo na Mipaka

Halmashauri ya Wilaya ya Rombo ni miongoni mwa Halmashauri sita (6) na Manispaa moja (1) zinazounda Mkoa wa Kilimanjaro ambazo ni; Hai, Same, Mwanga, Moshi, Siha na Manispaa ya Moshi.Wilaya hii ilianzishwa mwaka 1972.

Eneo la Wilaya ni kilomita za mraba 1,442 sawa na Hekta 144,000. Wilaya inapakana na nchi ya Kenya kwa upande wa Kaskazini na Mashariki. Upande wa Kusini na Kusini-Magharibi inapakana na Wilaya ya Moshi, Kaskazini-Magharibi inapakana na Wilaya za Siha na Longido iliyoko Mkoa wa Arusha.

Matumizi ya Ardhi

Hekta 44,114 ndizo zinafaa kwa Kilimo, Hekta 57 zinafaa kwa ufugaji, Hekta 38,194 ni misitu ya asili na ya kupandwa na hekta 16,492 zinafaa kwa malisho ya mifugo ,hekta 45,143 ni eneo la maji ,milima na miamba.

Utawala

Kiutawala Wilaya imegawanyika katika Tarafa 5, Kata 27, Vijiji 68 na Vitongoji 296. Aidha Kata moja ya Kelamfua Mokala imekuwa Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mkuu yenye jumla ya Mitaa 15. Wilaya ina Jimbo moja la Uchaguzi.

 

Hali ya Hewa

Wilaya ina majira ya Mvua za vuli yanayoanza mwezi Oktoba na kuishia mwezi Desemba na mvua za masika Machi hadi Mei na majira ya Kiangazi yanayoanza mwezi Juni na kuishia Oktoba. Wastani wa mvua kwa mwaka ni mm 1000 na wastani wa joto ni 220C. 

 

Wilaya imegawanyika katika kanda 3 ambazo ni:-

  • Ukanda wa Juu wenye udongo asili ya Volkano
  • Ukanda wa Kati wenye Udongo mchanganyiko wa mfinyanzi kidogo na tifutifu
  • Ukanda wa Chini wenye Udongo mchanganyiko wa mfinyanzi na kichanga pamoja na kiasi kidogo cha tifutifu.

 Idadi ya Watu

Idadi ya watu kwa mujibu wa Sensa ya Kitaifa ya Watu na Makazi mwaka 2012 Wilaya ina watu 260,963, Wanaume 124,528 na Wanawake 136,435 na wastani wa watu 4 kwa kila Kaya. Aidha uchambuzi wa taarifa mbalimbali za Sensa ikiwa ni pamoja na ongezeko la watu kwa mwaka unafanyika na Ofisi ya Taifa ya Takwimu.

 Shughuli za Kiuchumi 

Asilimia 90 ya wakazi wa Wilaya ya Rombo wanajishughulisha na kilimo na mifugo, asilimia 7 ni wafanyabiashara/wajasiriamali na asilimia 3 ni watumishi katika sekta mbalimbali za umma na binafsi. Pato la mwananchi kwa Wilaya ya Rombo ni Tshs 850,000/=kwa mwaka kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012.



Matangazo

  • MATOKEO YA USAHILI WA WALIOOMBA KAZI YA KUKUSANYA MAPATO NA KAZI YA USAFI August 27, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO June 14, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA August 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA July 16, 2024
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • Ona Zote

Video

Maafisa Elimu Kata wakizifanyia Majaribio Pikipiki
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Muundo wa Halmashauri
  • Wasiliana Nasi Kwa
  • Miladi iliyokamilika

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • MFUMO WA TAUSI
  • Ffars
  • Tamisemi
  • Idara ya Takwimu (NBS)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Rombo District Council,Mkuu Bomani Street

    Sanduku la Posta: P.o Box 52,Mkuu,Rombo

    Simu: 027-2757101

    Simu ya Mkononi: 027-2757101

    Barua Pepe: ded@rombodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright@2019Rombodc.all rights reserved