• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mipango na Takwimu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Afya
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • maji
    • Elimu
    • Watumishi
    • Kilimo
    • Afya
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti
    • Taratibu
    • Taarifa za Fedha
      • Taarifa ya makisio ya Mapato
      • Taarifa ya Mapato Halisi
      • Taarifa ya Matumizi
      • MTEF
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba

Tamaduni, chanzo cha ukatili wanawake,watoto

Posted on: March 7th, 2018

Picha kwa hisani ya mtandao

Tamaduni mbalimbali zinazojumuisha imani,maadili,sanaa,sheria, desturi na mila, ambazo nyingine ni za kigeni na nyingine ni za kitanzania huchangia kwa kiasi kikubwa ukatili dhidi ya wanawake na watoto,hayo yalibainishwa katika ufunguzi wa Kamati ya kupiga vita ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika wilaya ya Rombo na mtoa mada kutoka KWIECO(shirika lisilokuwa la kiserikali linalojihusisha na kuimarisha haki za binadamu na usawa wa kijinsia) Peter Mashingia.

Mashingia alisema kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake  na watoto inaenda sambamba na kutokomeza mila na desturi kandamizi ,aliziorodhesha  baadhi ya tamaduni  hizo kuwa ni ukeketaji, mila na desturi zinazohamasishaji mimba za utotoni ,mila na desturi zinazohamasisha ndoa za lazima  mtoto kuchaguliwa mme/mke akiwa shuleni, mume kumpiga mkewe kama ishara ya upendo.

‘ Tusijadili matokeo tuangalie nini hasa sababu ya haya matukio ya ukatili kutokea , wazazi wametawaliwa sana na shughuli za uchumi  badala ya  kusimamia makuzi  ya watoto nyumbani  na wengi wanaoleta haya matatizo ukichunguza anaishi na nani utakuta anaishi na babu au bibi,hivyo tunapozungumzia mazingira salama ni budi tujihoji wenyewe’. Mkuu wa Polisi Rombo  Joseph Marwa alichangia.

Marwa aliongeza kuwa “Utamaduni wa kigeni unaathiri sana katika makuzi ya watoto kuna matukio yanatokea kwa sababu tumeruhusu sana utamaduni wa kigeni utawale maisha yetu, kuna mila  ambazo wao wanaziona ni kandamizi lakini zilitusaidia na mimba za utotoni hazikuwepo”  

Alimalizia kwa kusema kuwa, ulinzi wa jamii kwa mtoto kwa nyakati hizi ni mgumu tofauti na zamani ambapo mtoto alikuwa ni wa jamii nzima hata akikosea anaadhibiwa lakini kwa sasa  ni ngumu kwa mtu kumchapa bakora mtoto wa jirani hata kama akimuona amekosea atajisemea shauri lake na wazazi wake.

Naye afisa maendeleo ya jamii wilaya Bi Restina Mwasha alisema timu zimeundwa kuanzia ngazi ya kijiji au mtaa kwa kujumuisha wataalamu kutoka sekta mbalimbali ili kufuatilia mnyororo mzima wa matukio ya ukatili yanayotokea katika maeneo yetu na kuyaripoti eneo husika.

Aliongeza kuwa huu ni mpango wa taifa uliopewa jina la MTAKUWWA (Mpango wa Taifa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto)ambao ni mpango utakaodumu kipindi cha miaka mitano kuanzia 2018 hadi 2022 lengo likiwa ni kutokomeza ukatili wa mama na mtoto kwa asilimia hamsini hivyo ili kuifikia asilimia hii ni budi ushiriki wetu uwe wa kina na matukio yaripotiwe.

Mbali na mikakati iliyowekwa na MTAKUWWA  kamati ya ulinzi wa wanawake na watoto imeundwa kwa kufuata mwongozo ili kuboresha utoaji wa huduma kwa makundi yaliyo katika mazingira hatarishi, kwa kutoa elimu na kuhamasisha jamii kuhusu kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto, ikiwa ni pamoja na kutoa msaada wa kisheria kwa waathirika wa ukatili na kuimarisha mahusiano katika jamii.




Matangazo

  • MATOKEO YA USAHILI WA WALIOOMBA KAZI YA KUKUSANYA MAPATO NA KAZI YA USAFI August 27, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO June 14, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA August 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA July 16, 2024
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • Ona Zote

Video

Maafisa Elimu Kata wakizifanyia Majaribio Pikipiki
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Muundo wa Halmashauri
  • Wasiliana Nasi Kwa
  • Miladi iliyokamilika

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • MFUMO WA TAUSI
  • Ffars
  • Tamisemi
  • Idara ya Takwimu (NBS)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Rombo District Council,Mkuu Bomani Street

    Sanduku la Posta: P.o Box 52,Mkuu,Rombo

    Simu: 027-2757101

    Simu ya Mkononi: 027-2757101

    Barua Pepe: ded@rombodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright@2019Rombodc.all rights reserved