• Contact us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Rombo District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • ujenzi
      • maji
      • Planning and Statitics
      • Livestock and Fishing
      • Community DEvelopment
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Ellimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Land and natural Resources
      • Human Resource and Administration
      • Health
    • Unit
      • ICT
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Law
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
    • Organisation Structure
  • Investiment Opportunities
    • Vivutio vya utalii
    • Industry
  • Our Services
    • Water
    • Elimu
    • Watumishi
    • Kilimo
    • Health
    • Mifugo
  • Councillors
    • List of Councillors
    • Permanent Commitees
    • Scheduals of Legal sessions
  • Projects
    • Completed projects
    • Ongoing projects
    • New Project
  • Publications
    • Forms
    • Acts
    • Report
    • Taratibu
    • Taarifa za Fedha
      • Taarifa ya makisio ya Mapato
      • Taarifa ya Mapato Halisi
      • Taarifa ya Matumizi
      • MTEF
    • Guidelines
  • Media Centre
    • Videos
    • News
    • Press Releae
    • Photo Gallery
    • Speech

Uharibifu wa chakula ni uhalifu-DC Hokororo

Posted on: November 1st, 2018

Mkuu wa wilaya ya Rombo Mhe. Agnes Hokororo  amepiga marufuku kwa wananchi kuruhusu mifugo kutoka nchi  jirani ya Kenya kufanya malisho mashambani  na kufanya uharibifu wa mazao ya chakula ,kwa sababu wakaazi wa Rombo wanafanya ufugaji  wa ndani  hivyo si vema kuruhusu mifugo ya watu wengine kuzurura.

Ameyasema hayo alipokuwa anasikiliza kero mbalimbali katika mkutano na wananchi wa kijiji cha Kiwanda mapema leo ,ambapo  wananchi walilalamika mazao yao kuliwa yakiwa shambani na mifugo kutoka nchi jirani ya Kenya ,na  wanapokuja kulisha mifugo wanakuja na silaha mbalimbali kama mapanga na sime.

Ameongeza kuwa pale inapotokea kuna makubaliano ya kibiashara ya kuuziana malisho kati ya Mkenya na Mtanzania basi ni vema aandaliwe kwa kukatiwa majani au mahindi na kupewa aondoke nayo ili kuepusha uharibifu wa mazao ya wengine mashambani kwa kuwa anapoingiza mifugo shambani hawafanyi malisho  eneo moja tu walilouziwa bali wanaharibu na mazao ya mashamba jirani.

“Uharibifu wa chakula ni uharibifu wa mali kama zilivyo mali zingine, Kaimu Kamanda wa Polisi wilaya nakuagiza, kama ambavyo tunakamata wahalifu katika maeneo mengine na hawa ni wahalifu vilevile kwasababu chakula ni hitaji muhimu katika jamii  kwa maendeleo ya kila siku”.alisema Hokororo

Pamoja na hilo ameushauri uongozi wa kijiji kuunda kamati imara ya kusimamia masuala ya mazingira ikiwa ni pamoja na  kuweka ulinzi wa kutosha kwa kila mtu kuwa mlinzi wa jirani yake ili kuwatambua wanaoruhusu malisho kwenye mashamba bila idhini ya wenye mashamba.

Wizara ilishatoa  onyo kuhusu mifugo kuzurura ovyo  pamoja na maelekezo ya kufuata sheria za NARCO ambazo zinaelekeza gharama za kuchangia mifugo inapofanya  uharibifu wa mazingira, nyasi walizokula , maji na mengineyo.

Kwa upande wa wanyama waharibifu kama Nyani,  Mhe. Hokororo amemuagiza Afisa Ardhi,maliasili na mazingira  kutafuta mbinu mbadala ya kuwafukuza bila kuwadhuru ili wasiendelee kuharibu mazao,

 Vile vile amewaelekeza wananchi pindi  wanyama wakubwa kama Tembo na wengine wanapokuja kushambulia basi ni budi kuandika barua kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ili wizara husika ipewe taarifa kwa ajili ya fidia inayotolewa kwa mujibu wa sheria

Matangazo

  • MATOKEO YA USAHILI WA WALIOOMBA KAZI YA KUKUSANYA MAPATO NA KAZI YA USAFI August 27, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO June 14, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA August 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI.

    May 29, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • View All

Videos

Maafisa Elimu Kata wakizifanyia Majaribio Pikipiki
More Videos

Kurasa za haraka

  • Muundo wa Halmashauri
  • Wasiliana Nasi Kwa
  • Miladi iliyokamilika

Kurasa za karibu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • MFUMO WA TAUSI
  • Ffars
  • Tamisemi
  • Idara ya Takwimu (NBS)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact us

    Rombo District Council,Mkuu Bomani Street

    Sanduku la Posta: P.o Box 52,Mkuu,Rombo

    simu: 027-2757101

    Mobile: 027-2757101

    staff mail: ded@rombodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Copyright@2019Rombodc.all rights reserved