• Contact us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Complaint |
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government Rombo District Council

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • ujenzi
      • maji
      • Planning and Statitics
      • Livestock and Fishing
      • Community DEvelopment
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Ellimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Land and natural Resources
      • Human Resource and Administration
      • Health
    • Unit
      • ICT
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Law
      • Internal Audit
      • Nyuki
      • Uchaguzi
    • Organisation Structure
  • Investiment Opportunities
    • Vivutio vya utalii
    • Industry
  • Our Services
    • Water
    • Elimu
    • Watumishi
    • Kilimo
    • Health
    • Mifugo
  • Councillors
    • List of Councillors
    • Permanent Commitees
    • Scheduals of Legal sessions
  • Projects
    • Completed projects
    • Ongoing projects
    • New Project
  • Publications
    • Forms
    • Acts
    • Report
    • Taratibu
    • Taarifa za Fedha
      • Taarifa ya makisio ya Mapato
      • Taarifa ya Mapato Halisi
      • Taarifa ya Matumizi
      • MTEF
    • Guidelines
  • Media Centre
    • Videos
    • News
    • Press Releae
    • Photo Gallery
    • Speech

Tamu na chungu ya Jani la Sale

Posted on: November 18th, 2019

Jani la sale ni maarufu miongoni mwa kabila la wachaga, ni jani linaloheshimika sana katika  kutatua migogoro na kuombea msamaha . Kwa imani za kichaga mtu yeyote aliyekosea akienda  kuomba msamaha na jani la sale basi ni budi asamehewe. Lakini pia jani hili hutumika kuwekea mipaka ya maeneo na kukaribishia wageni kama viongozi wa dini na serikali kuashiria amani .

Jani hili ambalo kwa uhalisia wake lilikua linasaidia kudumisha amani, upendo na mshikamano miongoni mwa kabila la wachaga limegeuka kuwa shubiri katika jamii ya wachaga kwasababu limekuwa likizorotesha  mchakato mzima wa kutafuta haki, na linachangia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa matendo ya ukatili pamoja na  mimba za utotoni.

Kamati ya MTAKUWWA( Mpango kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto) wilaya ya Rombo imeazimia  kuundwa kwa sheria ndogo dhidi ya matumizi ya  Jani la sale kwenye kesi za ukatili wa kijinsia, baada ya kuonekana kesi nyingi za ulawiti, ubakaji na mimba zinamalizwa kimila kwa kutumia majani hayo.

Aidha  baadhi ya wajumbe wa  kamati hiyo wamesema kuwa jani la sale limekuwa halitumiki tena kama jani la amani bali ni kama jani la kuvunia fedha,kwani katika mchakato wa kutatua kesi kimila sio jani la sale pekee linalotumika huwa linaambatana na fedha au mifugo ili mhusika kusamehewa.

Pamoja na hilo kuna baadhi ya wajumbe wa kamati ya MTAKUWWA walilishutumu jeshi la polisi wilaya ya Rombo kwa kuzorotesha upatikanaji wa haki kwa kutoshirikiana na wananchi kupinga vitendo vya ukatili kwa kuwaachia huru watuhumiwa.

Katika kujibu tuhuma hizo Mkuu wa Polisi (W) Ndg Ally Kitole ambaye ni mjumbe wa kamati hiyo, amesema kuwa hakuna kitu kinachomshangaza kama kesi za Jinai kutatuliwa kimila hasa kwa kutumia majani ya Sale, na kuongeza kuwa haki jinai haitegemei mtu mmoja kupatikana, na wananchi  ndio wamekuwa wakichangia kukwamisha mchakato mzima wa kupata haki , kwani muathirika mwenyewe ndio anakuwa wa kwanza kutotoa ushirikiano kwa jeshi la Polisi.

Naye Mkuu wa wilaya ya Rombo Mhe. Agness Hokororo akizungumza katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya wilaya kilichofanyika Nov,15 2019 ameelezea masikitiko yake juu ya kukithiri kwa vitendo vya ukatili na ukwamishaji wa haki pale ambapo wananchi wanakwamisha mchakato wa utafutaji wa haki kisheria.

 Amesema kuwa kesi nyingi za ulawiti na ubakaji katika mahakama ya wilaya zimeshindwa kuendelea kutokana na mzazi (mama) anapoitwa mahakamani kutoa ushahidi, wamekuwa wanaficha ukweli,hivyo kufifisha haki za watoto wao hasa pale wanapoamua kukubaliana na kumalizana na watuhumiwa.

Aidha Hokororo amezungumzia vitendo vya ukatili na mauaji ambavyo  vimekithiri katika wilaya ya Rombo hasa katika Tarafa ya Usseri ambapo kwa mwaka huu 2019 kuanzia Aprili hadi July  jumla ya watu wasiopungua  nane (8) waliuawa na kwa bahati mbaya jeshi la polisi lilishindwa kuhakikisha wahusika wanatiwa nguvuni  kwa sababu walikosa ushirikiano kutoka kwa wananchi.

Sambamba na hilo ameongelea matukio ya wanaume kujinyonga  katika eneo la Rombo , kitu ambacho pengine kwa kiasi kikubwa kinachangiwa na  vitendo vya ukatili na unyanyasaji wanavyofanyiwa wanaume, huku akisisitiza kuwa  matendo ya ukatili na unyanyasaji wanafanyiwa makundi yote hata wababa lakini hayaripotiwi.

Hokororo ametoa rai kwa viongozi wa dini wasisite kusemea  wazi wazi vitendo vya ukatili na unyanyasaji  katika makanisa na misikiti kwa kutumia maandiko ya dini  ili jamii ibadilike, kwa sababu matendo hayo ni kinyume na mpango wa Mungu.

 

Matangazo

  • MATOKEO YA USAHILI WA WALIOOMBA KAZI YA KUKUSANYA MAPATO NA KAZI YA USAFI August 27, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO June 14, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA August 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA July 16, 2024
  • View All

Habari Mpya

  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI.

    May 29, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • View All

Videos

Maafisa Elimu Kata wakizifanyia Majaribio Pikipiki
More Videos

Kurasa za haraka

  • Muundo wa Halmashauri
  • Wasiliana Nasi Kwa
  • Miladi iliyokamilika

Kurasa za karibu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • MFUMO WA TAUSI
  • Ffars
  • Tamisemi
  • Idara ya Takwimu (NBS)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact us

    Rombo District Council,Mkuu Bomani Street

    Sanduku la Posta: P.o Box 52,Mkuu,Rombo

    simu: 027-2757101

    Mobile: 027-2757101

    staff mail: ded@rombodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Sitemap

Copyright@2019Rombodc.all rights reserved