• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mipango na Takwimu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Afya
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • maji
    • Elimu
    • Watumishi
    • Kilimo
    • Afya
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti
    • Taratibu
    • Taarifa za Fedha
      • Taarifa ya makisio ya Mapato
      • Taarifa ya Mapato Halisi
      • Taarifa ya Matumizi
      • MTEF
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba

Rombo yatoa mkopo wa milioni 61.5 kwa vikundi 20

Posted on: January 10th, 2020

Halmashauri ya wilaya ya Rombo imetoa mkopo wa shilingi milioni 61.5  kwa  jumla ya vikundi  20, vya wanawake (12), Vijana ( 7) na wenye ulemavu ( 1), kupitia  10%(asilimia kumi) ya mapato ya ndani ,ambayo kwa mujibu wa sheria ni lazima  iende  kwenye makundi hayo ili kuyainua kiuchumi.

Afisa Maendeleo ya Jamii (W) Patricia Kinyange  ameeleza kuwa vikundi vilivyokuwa vimeomba mkopo vilikuwa 55 vilivyokuwa na thamani ya milioni 275  lakini  kutokana na mapato madogo ya Halmashauri  kamati ya wilaya ilikaa na kuchuja angalau kila Kata ipate kikundi kimoja na baada ya mchujo vilipatikana vikundi 20 ambavyo ndivyo vinavyopokea mkopo huo.

Ameongeza kuwa mikopo hii inayotolewa sasa ni ya kipindi cha robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha  2019/2020,  na hivi karibuni  halmashauri inategemea  kumalizia kutoa mikopo kwa  robo ya pili.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Rombo Mhe. Agness Hokororo  amevitaka vikundi vilivyopata mkopo kufanya biashara zao kwa kufuata sheria na taratibu huku wakijifunza kutunza akiba zao zitakazowasaidia kufanya uzalishaji mkubwa zaidi,  ili nia njema ya serikali ya kuwainua wananchi kiuchumi ionekane .

Sambamba na hilo  amewaasa  wanavikundi kujiepusha na biashara za magendo,  na  kuweka wazi iwapo wakijihusisha, serikali itawakamata na fedha yote ya kikundi itapotea na kuwasababishia hasara na kushindwa kufanya marejesho kitu kitakachopelekea Halmashauri kuwashitaki mahakamani.

“Natamani vikundi hivi viendelee kiuchumi na baadae hata kuungana na kuwa na mtaji mkubwa zaidi ili kuanzisha viwanda vitakavyokuwa vinatengeneza  bidhaa zilizoongezwa thamani  na bidhaa za uzalishaji ambazo zitakuwa zinatoka Rombo,” amezungumza Godwin Chacha ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Rombo.

Kabla ya kupewa mikopo hiyo vikundi hivyo vilipata mafunzo ya siku mbili juu ya uandaaji wa vitabu vya fedha vinavyotunza kumbukumbu, Elimu ya ujasiriamali,usimamizi wa akaunti , hatua za kuchukua kabla ya kuchukua mkopo, namna ya kufanya marejesho na jinsi ya kujisajili PPRA.


Matangazo

  • MATOKEO YA USAHILI WA WALIOOMBA KAZI YA KUKUSANYA MAPATO NA KAZI YA USAFI August 27, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO June 14, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA August 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA July 16, 2024
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • Ona Zote

Video

Maafisa Elimu Kata wakizifanyia Majaribio Pikipiki
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Muundo wa Halmashauri
  • Wasiliana Nasi Kwa
  • Miladi iliyokamilika

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • MFUMO WA TAUSI
  • Ffars
  • Tamisemi
  • Idara ya Takwimu (NBS)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Rombo District Council,Mkuu Bomani Street

    Sanduku la Posta: P.o Box 52,Mkuu,Rombo

    Simu: 027-2757101

    Simu ya Mkononi: 027-2757101

    Barua Pepe: ded@rombodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright@2019Rombodc.all rights reserved