• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali Za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Maji
      • Mipango na Takwimu
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
      • Utumishi na Utawala
      • Afya
    • Kitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Nyuki
      • Uchaguzi
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • maji
    • Elimu
    • Watumishi
    • Kilimo
    • Afya
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Mipya
  • Machapisho
    • Fomu
    • Sheria Ndogo
    • Ripoti
    • Taratibu
    • Taarifa za Fedha
      • Taarifa ya makisio ya Mapato
      • Taarifa ya Mapato Halisi
      • Taarifa ya Matumizi
      • MTEF
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba

RC BABU AIPONGEZA ROMBO KWA KUPATA HATI SAFI KWA MARA YA TATU MFULULIZO

Posted on: July 4th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin babu amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rombo Ndg Godwin Chacha na menejimenti ya Halmashauri kwa kuvuka lengo katika ukusanyaji wa mapato kwa asilimia 118 kwa mwaka wa fedha 2023/24



Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ameipongeza Wilaya ya Rombo kwa kupata hati safi kwa miaka mitatu mfulululizo.

Akizungumza wakati wa mkutano maalum wa kujadili hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa Hesabu za serikali leo Julai 04, 2024 uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauri, Mhe Nurdin Babu amesema Wilaya ya Rombo inachangia kwa kiasi kikubwa Mkoa wa Kilimanjaro kuendelea kufanya vizuri kitaifa.

Mhe Nurdin Babu amewaelekeza Mwenyekiti wa Halmashauri, Mkurugenzi Mtendaji na Waheshimiwa madiwani kuendelea kusimamia na kuhakikisha hakuzalishwi hoja zaidi ya kumi wakati wa ukaguzi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali – CAG Mwaka 2024/2025.



“Nataka wakuu wa idara wote washiriki kikamilifu katika suala zima la kuzuia uwepo wa hoja na kuzijibu hoja za ukaguzi, nyinyi wakuu wa idara ndio tunawategemea, muwasaidie sana waheshimiwa madiwani kuchakata na kujibu hoja zote kwa ufanisi kama mlivyofanya sasa” amesema Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu.



“Mkurugenzi endeleeni kumuwezesha Mkaguzi wa Ndani afanye kazi yake, kwa sababu yeye ndio anajua hili tusipolitekeleza itakuwa hoja na tukitekeleza haitakuwa hoja kwa hiyo msaidieni mkaguzi wa ndani” ameongeza Mhe Nurdin Babu.



Kikao hicho cha kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali – CAG kimefanyika ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Rombo imewasilisha hoja tano za ukaguzi zilizojadiliwa na kutolewa maelekezo na waheshimiwa madiwani mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe Nurdin Babu.



Matangazo

  • MATOKEO YA USAHILI WA WALIOOMBA KAZI YA KUKUSANYA MAPATO NA KAZI YA USAFI August 27, 2024
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA VYA HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO June 14, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA August 26, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA AJIRA YA MKATABA July 16, 2024
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • KARIBU KWENYE BARAZA LA MADIWANI.

    May 07, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • ZAID YA SHILINGI MILIONI MIA SITA AROBAINI NA MOJA YA KABIDHIWA KWA VIKUNDI 52

    April 17, 2025
  • Ona Zote

Video

Maafisa Elimu Kata wakizifanyia Majaribio Pikipiki
Video Zaidi

Viunganishi Vya Haraka

  • Muundo wa Halmashauri
  • Wasiliana Nasi Kwa
  • Miladi iliyokamilika

Viunganishi Linganifu

  • Ikulu
  • Utumishi
  • MFUMO WA TAUSI
  • Ffars
  • Tamisemi
  • Idara ya Takwimu (NBS)

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Rombo District Council,Mkuu Bomani Street

    Sanduku la Posta: P.o Box 52,Mkuu,Rombo

    Simu: 027-2757101

    Simu ya Mkononi: 027-2757101

    Barua Pepe: ded@rombodc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Copyright@2019Rombodc.all rights reserved